Jumanne 5 Agosti 2025 - 21:07
Sheikh Zakzaky awapokea mazuwari wa Kinigeria kabla ya kuondoka kuelekea matembezi ya Arubaini ya Husein (as)

Hawza/ Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria, Ibrahim Zakzaky, amewapokea mahujaji wote wa Nigeria wanaokusudia kuelekea Karbala katika siku za Arubaini ya Husein, kabla ya kuondoka kwao kuelekea Karbala.

Kwa mujibu wa ripoti ya kikundi cha tarjuma cha Shirika la Habari la Hawza, Sheikh Ibrahim Zakzaky, kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria, amewapokea mazuwari wa Arubaini wa Nigeria, na katika hotuba yake iliyosadifiana na tarehe 8 mwezi wa Safar, alisisitiza umuhimu wa matembezi ya Arubaini na kusema kuwa mkusanyiko huu mkubwa katika njia ya Najaf kuelekea Karbala ni matokeo ya mafundisho ya Imam Husein (as) na Ahlul-Bayt (as).

Aidha, alizungumzia kuhusu tukio la Karbala na kusema: Uadui kati ya Bani Umayyah, Yazid na wafuasi wao haujawahi kupunguza hata chembe ya mapenzi ya Ahlul-Bayt (as) katika nyoyo za Mashia na wapenzi wao.

Sheikh Zakzaky awapokea mazuwari wa Kinigeria kabla ya kuondoka kuelekea matembezi ya Arubaini ya Husein (as)

Baadhi ya washiriki waliokuwa wakifuatilia kwa karibu Hotuba ya Sheikh Zakzaky

Sheikh Zakzaky alisema: Wale wanaotekeleza mauaji ya kimbari katika historia watalaaniwa milele, kuanzia Firauni aliyefanya kitendo hiki kibaya katika zama za kale, hadi kwa wahalifu wa leo.

Mwishoni, kiongozi wa Harakati ya Kiislamu aliuombea dua msafara huo kwa kusema: Inshaallah, Mwenyezi Mungu Mtukufu aufanye msafara huu wa mazuwari uwe salama.

Chanzo: Tovuti rasmi ya Harakati ya Kiislamu ya Nigeria.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha